Search This Blog

March 29, 2013

TAASISI YA CATHERINE FOUNDATION DEVELOPMENT YATOA MISAADA YA KIJAMII KWA WAGONJWA NA WATOTO YATIMA ARUSHA JANA.


Taasisi ya Maendeleo isiyo ya kiserikali ya Catherine Foundation ya jijini Arusha leo imetoa misaada mbalimbali ya vyakula kwa wagonjwa Hospitali ya Mt Meru na vituo viwili vya Yatima vya Faraja na Lohada Moshono vyopte vya jijini humo.

Catherine Foundation Develeppent inaongozwa na Mbunge wa Viti Maalum UVCCM Arusha, Catherine Magigie.

Misaada hiyo ya vyakula na sabuni pamoja na kuwatembelea wagonjwa kufanyika ikiwa ni sehemu ya kuwapa faraja wagonjwa na yatima hao waki huu wa kuelekea siku kuu ya Pasaka ili nawao wajisikie ni miongoni mwa jamii.
Mbunge wa Viti Maalum, Catherine Magige ambaye ni Kiongozi wa Taasisi ya Catherine Foundation, akimkabidhi  Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mount Meru, Frida Mokit msaada wa mablang’eti ya kujifunikia wagonjwa waliolazwa Hospitalini hapo.
Mbunge wa Viti Maalum, Catherine Magige ambaye ni Kiongozi wa Taasisi ya Catherine Foundation, akiwajulia hali wagonjwa waliolazwa Hospitali ya Mt. Meru ya jijini Arusha na kuwapa zawadi mbalimbali.
Ilikuwa ni uchungu sana kwa Mbunge wa Viti Maalum, Catherine Magige ambaye ni Kiongozi wa Taasisi ya Catherine Foundation, alipopata taarifa za watoto zaidi ya 200 wanao lelewa katika kituo cha Yatima cha Faraja mjini Arusha. Watoto hao ni yatima ambao walitelekezwa na wazazi wao maeneo mbalimbali mjini humo na wengine ni waathirika wa Virusi vya Ukimwi. Mtoto aliyempakata alitupwa jalalani na wazazi wake angali mchanga na kulelewa hadi umri huo Hospitalini hapo.
Mbunge Catherine Magige ambaye ni Kiongozi wa Taasisi ya Catherine Foundation, akimkabidhi  Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mount Meru, Frida Mokit msaada wa vitu mbalimbali kwaajili ya wagonjwa waliolazwa Hospitalini hapo.
Wanachama wa CCM na Taaasisi ya Catherine Foundation Development inayoongozwa na Mbunge wa Viti Maalum Arusha, Catherine Magige wakiwa wamebeba zawadi mbalimbali wakielekea katika moja ya wodi za akina mama na watoto Hospitali ya Mount Meru jijini Arusha kukabidi zawadi hizo.

Mbunge Catherine Magige akiongozana na Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mount Meru, Frida Mokit wakifutana na wana Catherine  Foundation wakielekea kwenye moja ya wodi za wagonja hospitalini hapo kutoa misaada.
Mbunge wa Viti Maalum, Catherine Magige ambaye ni Kiongozi wa Taasisi ya Catherine Foundation, akiwa amewapakata watoto wawili mapacha waliozaliwa katika Hospitali ya Mount Meru jijini Arusha.
 
 Mbunge wa Viti Maalum, Catherine Magige ambaye ni Kiongozi wa Taasisi ya Catherine Foundation, akisoma taarifa yake na kuzungumza na watu mbalimbali wakiwapo wafanyakazi wa Hospitali ya Mount Meru.
SOURCE: MROKI MROKI

No comments:

Post a Comment

ABUSIVE LANGUAGE IS NOT ALLOWED TO THIS BLOG. THANK U FOR UR COOPERATION

Note: Only a member of this blog may post a comment.

YOU MAY ALSO LIKE THIS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...